• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yapokea walimu 50 kutoka Zanzibar

Posted on: September 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewapokea walimu zaidi ya 50 kutoka Chama cha Walimu Zanzibar walio katika ziara ya mafunzo na utalii katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza na walimu hao, Mheshimiwa Mzee amewapongeza walimu hao kwa kufanya utalii wa ndani na kuchagua kuutembelea Mkoa wa Mara wenye vivutio vingi vya utalii na kihistoria ya Taifa letu. 

“Mara ni sehemu ambayo ina vivutio vingi vya asili ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuongeza kuwa Mara ndio chimbuko la Tanzania” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara amefurahi sana kuona walimu hao wamekuja kufanya utalii na kujifunza katika Mkoa wa Mara na kuwataka warudi Mara watakapojisikia uchovu na msongo wa mawazo.  

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Mara ambaye ni mwenyeji wa walimu hao Bibi Suzan Shesha amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuweza kuonana na walimu hao pamoja na ratiba za shughuli zake kuwa nyingi.

“Sisi pamoja na wageni wetu tunashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuweza kukutana na walimu hawa, na tunakuahidi tutawatembeza maeneo yote watakayotaka kwenda na kuwapa ushirikiano wakati wote wakiwa katika Mkoa wa Mara” alisema Bibi Shesha.  

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) Bwana Musa Abdi Hamis ameeleza kuwa ziara yao pamoja na kujifunza kutoka katika shule mbalimbali za Mkoa wa Mara, watatembelea vivutio vya utalii na nyumbani kwa Baba wa Taifa ili kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhamasisha utalii kupitia filamu ya Royal Tour.

Bwana Hamis ameeleza kuwa katika ziara hiyo, watatembelea shule mbalimbali za msingi, shule za sekondari zinazofanya vizuri sana na zile ambazo hazifanyi vizuri katika mitihani ya Taifa ili kuweza kujifunza.

Aidha, walimu hao wanatarajia kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, maonyesho ya Mara International Expo yanayoendelea katika viwanja vya Mukendo, Manispaa ya Musoma, mpaka wa Tanzania na Kenya uliopo eneo la Sirari wilayani Tarime, Shule ya Msingi Mkendo aliyosoma Baba wa Taifa na nyumbani kwa Baba wa Taifa.

Walimu hao pia walitoa zawadi za viungo vya Zanzibar mbalimbali kwa Mkuu wa Mkoa na Chama cha Walimu Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • RC Ampokea Meja Jenerali Mani

    May 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa